Tombo
Tombo | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
|
Tombo (pia tomboo au tomboro) ni ndege wadogo wa jenasi kadhaa katika familia ya Phasianidae. Rangi yao ni kahawia na wana michirizi. Spishi nyingine zina rangi nyekundu na buluu. Kabla ya kuruka angani hungoja mpaka mtu ni karibu kuwakanyaga na huenda umbali fupi tu. Hula mbegu hasa lakini pengine hukamata wadudu pia. Hutaga mayai 6-18 ardhini.
Tombo wanatokea Afrika, Australasia na Ulaya. Kuna ndege huko Amerika ambao wana mnasaba na tombo, lakini wanaainishwa ndani ya familia Odontophoridae.
Spishi za AfrikaEdit
- Coturnix coturnix, Tombo wa Ulaya (Common Quail)
- Coturnix c. africana, Tombo wa Afrika (African Quail)
- Coturnix c. coturnix, Tombo wa Ulaya (Eurasian Quail)
- Coturnix c. erlangeri, Tombo Habeshi (Abyssinian Quail)
- Coturnix c. inopinata, Tombo wa Kaboverde (Cape Verde Quail)
- Coturnix delegorguei, Tombo Kidari-cheusi (Harlequin Quail)
- Excalfactoria adansonii, Tombo Buluu (Blue Quail)
- Perdicula asiatica, Tombo wa Asia (Jungle Bush-quail) imewasilishwa katika Reunion
Spishi za mabara mengineEdit
- Anurophasis monorthonyx (Snow Mountain Quail)
- Coturnix coromandelica (Rain Quail)
- Coturnix japonica (Japanese Quail)
- Coturnix novaezelandiae (New Zealand Quail) imekwisha sasa
- Coturnix pectoralis (Stubble Quail)
- Coturnix ypsilophora (Brown Quail)
- Excalfactoria chinensis (King Quail)
- Ophrysia superciliosa (Himalayan Quail) labda imekwisha sasa
- Perdicula argoondah (Rock Bush Quail)
- Perdicula asiatica (Jungle Bush Quail)
- Perdicula erythrorhyncha (Painted Bush Quail)
- Perdicula manipurensis (Manipur Bush Quail)