Yohane Boste (Dufton, Westmorland, Uingereza, 1544 hivi – Dryburn, Durham, 24 Julai 1594) aliwahi kuwa mhubiri wa Kanisa la Anglikana kabla hajarudi katika Kanisa Katoliki mwaka 1576 akiwa mwalimu mkuu tayari.

Baada ya kuhamia Ufaransa, aliingia seminari kwa kengo la kurudi kwao kufanya uchungaji usioruhusiwa na serikali, akapewa daraja ya upadri huko Reims (Machi 1581).

Mwezi uliofuata alirudi Uingereza na kufanya utume wake kwa siri hadi aliposalitiwa na kukamatwa mwaka 1593. Chini ya malkia Elizabeti I aliteswa kikatili mara 15 asiweze tena kutembea bila mkongojo. Mwaka uliofuata alinyongwa na kukatwa vipandevipande akiwa bado hai. Hata mbele ya hakimu hakuacha kuwatia moyo wafungwa wenzake[1].

Papa Paulo VI tarehe 25 Oktoba 1970 alimtangaza kuwa mtakatifu mfiadini pamoja na wenzake 39.

Sikukuu yake ni tarehe 24 Julai[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.