Amato Ronconi (Saludecio, Rimini, Italia, 1225 hivi - Saludecio, 8 Mei 1292 hivi) alikuwa Mkristo maarufu kwa kuishi miaka mingi kwa toba na hija. Alijenga makanisa na vituo vya kuhudhumia kwa ukarimu mkubwa wasafiri na maskini, ambao aliwagawia mali yake yote[1].

Mtakatifu Amato alivyochorwa.

Kwa sababu hizo, wengine wanasema alikuwa Mfransisko wa Utawa wa Tatu[2].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu. Hiyo ilithibitishwa kwanza na Papa Pius VI tarehe 17 Aprili 1776, halafu na Papa Fransisko tarehe 23 Novemba 2014[3].

Sikukuu yake ni tarehe 8 Mei[4].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.