Arusha Poetry Club

Arusha Poetry Club (inajulikana zaidi kama APC) ni moja ya majukwaa ya kwanza ya washairi kama yalivyo majukwaa mengi ya sanaa ya ushairi ambayo yalianzishwa kwa lengo la kuendeleza sanaa nchini Tanzania. APC ina washairi wengi wa aina tofautitofauti, wakubwa kwa wadogo.

Historia hariri

Historia ya sanaa ya ushairi Tanzania imeanza miaka, toka enzi zile za washairi wakubwa kama kina Shaaban Robert na wengine ambao ndio magwiji wa ushairi.

APC ilianzishwa tarehe 1 Septemba 2012 na mshairi George Kyomushula[1] kwa kushirikiana na Charlotte Hill O'Neal mwana diaspora kutokea Amerika .

Lengo la kundi hili lilikuwa kuwakutanisha washairi na wapenzi wa mashairi toka pande mbalimbali za Tanzania na dunia.

Arusha Poetry Club ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwakutanisha washairi toka nchi za Kenya, Marekani, Israel, Ufaransa na nchi nyingine.

APC ni mojawapo ya majukwaa ya washairi ambayo yamewahi kufanya matamasha mengi ya washairi katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam na Mwanza

Wanachama maarufu hariri

Arusha Poetry Club ina wanachama wengi ambao ni maarufu katika uandishi wa mashairi na vitabu vya aina tofauti tofauti kama:

Tanbihi hariri

  1. Tanzania: Arusha Poetry Club 'Puts Pains On Minds', taarifa kwenye tovuti ya Allafrica,com ya tar. 3 Julai 2013, iliangaliwa kwenye Agosti 2018

Viungo vya nje hariri