Mkoa wa Dar es Salaam


Dar es Salaam ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepakana na Mkoa wa Pwani pande zote barani na Bahari ya Hindi upande wa mashariki.
Eneo la mkoa ni jiji la Dar es Salaam ambalo ndilo kitovu cha shughuli za biashara (na za utawala, kwa kiasi fulani) nchini Tanzania, na ni kati ya majiji yanayokua haraka zaidi duniani.
Ni km² 1,800 pamoja na visiwa vidogo 8 na eneo la bahari kati ya pwani na visiwa hivi. Eneo la nchi kavu pekee ni km² 1,393.
Kuna wilaya tano: Kinondoni (wakazi 1,775,049), Ilala (wakazi 1,220,611) na Temeke (wakazi 1,368,881) ambazo zimeongezewa Kigamboni na Ubungo. Kila moja inaangaliwa kama mji. Takwimu hizi ni za mwaka 2012, kwa ujumla idadi ya wakazi ilikuwa 4,364,541.
Wakazi asili wa eneo la mkoa walikuwa Wazaramo pamoja na makabila madogo kama vile Wandengereko na Wakwere. Kutokana na kukua na kupanuka kwa jiji kuna makabila yote.
Majimbo ya bungeEdit
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Ilala : mbunge ni Mussa Azzan Zungu (CCM)
- Kawe : mbunge ni Halima Mdee (Chadema)
- Kibamba : mbunge ni John John Mnyika (Chadema)
- Kigamboni : mbunge ni Faustine Ndugulile (CCM)
- Kinondoni : mbunge ni Maulid Mtulia (CCM)
- Mbagala : mbunge ni Issa Ally Mangungu (CCM)
- Segerea : mbunge ni Bonna Mosse Kaluwa (CCM)
- Temeke : mbunge ni Abdallah Mtolea (CUF)
- Ubungo : mbunge ni Saed Kubenea (Chadema)
- Ukonga : halina mbuge kwa sasa.
Tazama piaEdit
Viungo vya njeEdit
- Sensa ya 2002
- (Kiingereza)Usalama katika Daressalaam
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Geita | Iringa | Kagera | Katavi | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Njombe | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Simiyu | Singida | Songwe | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |