Mkoa wa Dar es Salaam

Mkoa wa Dar es Salaam ni mojawapo ya mikoa ya Tanzania ulioko katika pwani ya mashariki mwa Tanzania. Unapakana na Mkoa wa Pwani upande wa magharibi, kaskazini, na kusini, huku upande wa mashariki ukipakana na Bahari ya Hindi. Ni mkoa mdogo zaidi kwa ukubwa wa eneo (km² 1,393 pamoja na visiwa vidogo 8), lakini una idadi kubwa zaidi ya wakazi nchini, ukiwa na watu takriban 5,383,728 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022,[1] tena ni kati ya majiji yanayokua haraka zaidi duniani. Ingawa Dodoma ni mji mkuu wa kisiasa, Dar es Salaam inabaki kuwa makao makuu ya taasisi nyingi za serikali, mashirika ya kimataifa, na sekta binafsi. Pia ni kitovu cha shughuli za biashara, uchumi, na usafirishaji nchini, na inahudumia pia nchi za jirani kupitia bandari ya Dar es Salaam.Mkoa huu una wilaya tano: Ilala, Kinondoni, Temeke, Ubungo, na Kigamboni.

Mahali pa Mkoa wa Dar es Salaam katika Tanzania.
Dar es Salaam miaka ya 1930.
Uwanja wa Taifa
Machweo jijini
Ghorofa ndefu kuliko zote za Afrika Mashariki.
Makao makuu ya Benki kuu ya Tanzania.
Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Shamba la Mungu.

Wakazi asili wa eneo la mkoa ni Wazaramo ingawa kwa sasa kutokana na kukua na kupanuka kwa jiji, kuna makabila yote ya Tanzania, mbali ya wageni wengi kutoka nchi mbalimbali.

Majimbo ya bunge

hariri

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2020 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri

Viungo vya nje

hariri