Mkoa wa Mwanza
Mkoa wa Mwanza ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania, wenye postikodi namba 33000. Umepakana na Geita upande wa magharibi, Shinyanga na Simiyu upande wa kusini na Mara upande wa mashariki. Ziwa la Viktoria Nyanza liko kaskazini.
Mkoa wa Mwanza |
|
![]() |
|
Majiranukta: 2°45′S 32°45′E / 2.750°S 32.750°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Wilaya | 8 |
Mji mkuu | Mwanza |
Serikali | |
- Mkuu wa Mkoa | Abas Kandoro |
Eneo | |
- Jumla | 19,592 km² |
Idadi ya wakazi (2002) | |
- Wakazi kwa ujumla | 3,699,872 |
Tovuti: http://www.mwanza.go.tz/ |

Makao makuu ya mkoa yapo Mwanza mjini.
Mkoa una wakazi 3,699,872 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1].
Wilaya Edit
Kabla ya kumegwa na kuzaa mkoa mpya wa Geita, mkoa wa Mwanza ulikuwa na wakazi 2,942,148 (sensa ya mwaka 2002) katika wilaya 8 ukiwa na eneo la 19,592 km2.
Wilaya ndizo Ukerewe, Magu, Sengerema, Geita, Misungwi, Kwimba, Nyamaganga na Ilemela. Jiji la Mwanza ndani yake lina wilaya za Nyamagana na Ilemela.
Ramani (kabla ya 2012) | Wilaya au manisipaa | Wakazi (2002) | Tarafa | Kata | Kijiji | Eneo km² |
---|---|---|---|---|---|---|
Wilaya ya Ilemela | 265,911 | |||||
Wilaya ya Kwimba | 316,180 | |||||
Wilaya ya Magu | 416,113 | |||||
Wilaya ya Misungwi | 257,155 | |||||
Wilaya ya Nyamagana | 210,735 | |||||
Wilaya ya Sengerema | 501,915 | |||||
Wilaya ya Ukerewe | 261,944 | |||||
Jumla | 2,942,148 | 19,592 | ||||
Mkoa wa Mwanza una Halmashauri za Wilaya tatu sita ambazo ni Geita, Sengerema, Magu, Misungwi, Kwimba na Ukerewe na Halmashauri ya Jiji la Mwanza inayohudumia wilaya za Nyamagana na Ilemela. | ||||||
Marejeo: Mkoa wa Mwanza |
Wakazi Edit
Makabila makubwa ya Mwanza ndio Wasukuma na Wazinza upande wa bara, halafu Wakerewe na Wakara visiwani.
Majimbo ya bunge Edit
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Buchosa : mbunge ni Dk. Charles Tizeba (CCM)
- Ilemela : mbunge ni Angelina Mabula (CCM)
- Kwimba : mbunge ni Mansoor Hirani (CCM)
- Magu : mbunge ni Kiswaga Boniventura (CCM)
- Misungwi : mbunge ni Charles Kitwanga (CCM)
- Nyamagana : mbunge ni Stanslaus Mabula (CCM)
- Sengerema : mbunge ni William Ngeleja (CCM)
- Sumve : mbunge ni Richard Mganga Ndassa (CCM)
- Ukerewe : mbunge ni Joseph Mkundi (CCM)
Tazama pia Edit
Tanbihi Edit
Viungo vya nje Edit
- Tovuti rasmi ya Mkoa wa Mwanza
- Mji wa Mwanza, habari za uchumi, utamaduni na mengi mengine Archived 11 Mei 2008 at the Wayback Machine.
- Matokeo ya Sensa 2002 kwa Mwanza* Serikali ya TanzaniaArchived 15 Desemba 2003 at the Wayback Machine.
- Wasukuma Archived 3 Julai 2008 at the Wayback Machine.
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Geita | Iringa | Kagera | Katavi | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Njombe | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Simiyu | Singida | Songwe | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mwanza bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Mwanza kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno. |