Mkoa wa Mwanza

Mkoa wa Tanzania


Mkoa wa Mwanza ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania, wenye postikodi namba 33000.

Mkoa wa Mwanza
Mahali paMkoa wa Mwanza
Mahali paMkoa wa Mwanza
Mahali pa Mkoa wa Mwanza katika Tanzania
Majiranukta: 2°45′S 32°45′E / 2.750°S 32.750°E / -2.750; 32.750
Nchi Tanzania
Wilaya 8
Mji mkuu Mwanza
Serikali
 - Mkuu wa Mkoa Abas Kandoro
Eneo
 - Jumla 19,592 km²
Idadi ya wakazi (2022)
 - Wakazi kwa ujumla 3,699,872
Tovuti:  http://www.mwanza.go.tz/
Mwanza

Umepakana na Geita upande wa magharibi, Shinyanga na Simiyu upande wa kusini na Mara upande wa mashariki. Ziwa la Viktoria Nyanza liko kaskazini.

Makao makuu ya mkoa yapo Mwanza mjini.

Mkoa una wakazi 3,699,872 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1].

Kabla ya kumegwa na kuzaa mkoa mpya wa Geita, mkoa wa Mwanza ulikuwa na wakazi 2,942,148 (sensa ya mwaka 2002) katika wilaya 8 ukiwa na eneo la 19,592 km2.

Wilaya hariri

Wilaya ndizo Ukerewe, Magu, Sengerema, Buchosa, Misungwi, Kwimba, Nyamagana na Ilemela. Jiji la Mwanza ndani yake lina wilaya za Nyamagana na Ilemela.

Ramani (kabla ya 2012) Wilaya au manisipaa Wakazi (2022) Tarafa Kata Kijiji Eneo km²
 
Wilaya za Mkoa wa Mwanza
Wilaya ya Buchosa 413,110
Wilaya ya Ilemela 509,687
Wilaya ya Kwimba 480,025
Wilaya ya Magu 421,119
Wilaya ya Misungwi 467,867
Wilaya ya Nyamagana 594,834
Wilaya ya Sengerema 425,415
Wilaya ya Ukerewe 387,815
Jumla 3,699,872
Marejeo: Mkoa wa Mwanza

Wakazi hariri

Makabila makubwa ya Mwanza ndio Wasukuma na Wazinza upande wa bara, halafu Wakerewe na Wakara visiwani.

Majimbo ya bunge hariri

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

Tazama pia hariri

 
Mwamba wa Bismarck ziwani.

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mwanza bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Mwanza kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.