Barbara Kaija

Mwandishi wa habari wa Uganda na mwalimu (alizaliwa 1964)

Barbara Kaija (alizaliwa 1964) ni mwandishi wa habari na mwalimu wa Uganda, ambaye ni mhariri mkuu wa kituo cha habari cha Vision Group na magazeti, pamoja na chapisho la kila siku la Kiingereza "New Vision".[1]

Barbara Kaija
Nchi Uganda
Majina mengine Barbara Kaija
Kazi yake ni mwandishi wa habari na mwalimu wa Uganda
Cheo uandishi wa habari za maendeleo
Ndoa Barbara Kaija ameolewa

Maisha ya awali na elimu hariri

Alisoma katika Chuo Kikuu cha Makerere, chuo kikuu kikongwe cha umma cha Uganda, alihitimu Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Elimu. Ikifwatiwa na shahada ya uzamili ya Sanaa katika elimu, chuo kikuu cha Makerere. Baadaye, alipata shahada ya uzamili wa Sanaa katika uandishi wa habari na masomo ya habari, kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, huko, Afrika Kusini. Pia ana Stashahada ya Uandishi wa Habari wa Vitendo, aliyoipata Cardiff, nchini Uingereza, chini ya ufadhili wa Thomson Foundation.[2]

Kazi hariri

Alifanya kazi katika Vision Group kwa zaidi ya miaka 25. Mnamo 1992, aliajiriwa kama mkufunzi wa wahariri wadogo. Baada ya muda, alipewa majukumu zaidi na akapandashwa cheo na kua Mhariri wa Makala ya Naibu. Baadaye alikua Mhariri wa Vipengele, akihudumu katika nafasi hiyo kwa miaka kumi. Aliteuliwa kuwa naibu Mhariri Mkuu mnamo 2006 na alikua Mhariri Mkuu mwaka 2010. Kutokana na uwezo wake wa sasa, anasimamia viwango vya uandishi wa habari na mkakati wa majukwaa yote ya media (magazeti, redio, televisheni, mtandao na media ya kijamii).Alipochukua nafasi ya Mhariri Mkuu mwaka 2010, alikua mwanamke wa kwanza wa Uganda kuwa mhariri mkuu wa gazeti kuu la Uganda katika historia ya nchi hiyo..[3]

Utambuzi hariri

Barbara Kaija ana shauku ya uandishi wa habari na kujitolea kufundisha wengine. Amebobea katika "uandishi wa habari za maendeleo", ambamo amefundisha na kusimamia waandishi wa habari wengi wa Uganda. Mnamo mwaka wa 2012, alipewa tuzo ya "Jubilee ya Kitaifa", kwa kutambua kazi yake.[2] In March 2011, the Ugandan newspaper Daily Monitor, part of the Aga Khan-owned Nation Media Group, named her one of "Today's Uganda Top Fifty Women Movers".[3]

Maisha binafsi hariri

Barbara Kaija ameolewa.[2] Amezaliwa mara ya pili na kwa sasa imani ya Kikristo inaongoza maisha yake.

Viungo vya Nje hariri

Marejeo hariri

  1. Mary Karugaba, and Carol Natukunda (18 March 2016). New Vision celebrates 30 years. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-05-11. Iliwekwa mnamo 4 November 2017.
  2. 2.0 2.1 2.2 NVG (206). New Vision Group: Senior Management. New Vision Group (NVG). Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-09-04. Iliwekwa mnamo 4 November 2017.
  3. 3.0 3.1 Today's Uganda top fifty women movers (8 March 2011). Iliwekwa mnamo 4 November 2017.
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Barbara Kaija kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.