Bruno wa Wurzburg

chansela mkuu

Bruno wa Wurzburg (1005 hivi - Persenbeug, Austria ya Chini, 27 Mei 1045) alikuwa chansela wa Italia (1027-1034) kwa niaba ya ndugu yake kaisari Konrad II, halafu askofu na mtawala wa Wurzburg hadi kifo chake[1][2].

Mt. Bruno katika dirisha la kioo cha rangi.

Alikarabati kanisa kuu, alirekebisha maisha ya kleri na kuwafundisha waumini Maandiko Matakatifu[3].

Bruno aliandika pia kitabu cha ufafanuzi wa Zaburi na tenzi kumi za Biblia, kwa kutumia madondoo ya Mababu wa Kanisa.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 27 Mei[4].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Schütz, Markus. "St. Burkard – das erste Kloster in Würzburg – Geschichte (German)". Haus der Bayerischen Geschichte – Klöster in Bayern. Iliwekwa mnamo 1 February 2018.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Lins, Joseph. "Diocese of Würzburg." The Catholic Encyclopedia Vol. 15. New York: Robert Appleton Company, 1912. 10 June 2018
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/54850
  4. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • Peter Kolb and Ernst-Günther Krenig (eds.), 1989: Unterfränkische Geschichte, pp. 229–232. Würzburg

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.