Ewostatewos (kwa Kigeez: ኤዎስጣቴዎስ, ʾĒwōsṭātēwōs, au ዮስጣቴዎስ, Yōsṭātēwōs, kutoka Kigiriki Εὐστάθιος, Eustathios; 15 Julai 127315 Septemba 1352 kadiri ya Kalenda ya Juliasi) alikuwa mmonaki, mwalimu wa Absadi.

Alidai utekelezaji wa Sabato pamoja na Dominika katika Ukristo wa Ethiopia. Hatimaye wafuasi wake walifaulu kufanya msimamo huo ukubaliwe mwaka 1450 kwenye Mtaguso wa Debre Mitmaq huko Tegulet.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa la Kiorthodoksi la Ethiopia na Kanisa la Kiorthodoksi la Eritrea kama mtakatifu.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Chanzo hariri

  • Holweck, F. G. A Biographical Dictionary of the Saints. St. Louis, MO: B. Herder Book Co. 1924.
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.