Fransisko wa Laval

Fransisko wa Laval (Montigny-sur-Avre, Perche, 30 Aprili 1623 - Quebec, 6 Mei 1708), alikuwa askofu Mfaransa, wa kwanza katika koloni la New France, ambayo sasa ni sehemu ya Québec, Kanada, na mwanzilishi wa Shirika La Notre Dame wa Montreal.

Mt. Fransisko wa Laval.

Aliweka makao makuu katika jiji la Quebec na kwa miaka 50 hivi alistawisha Kanisa Katoliki katika Amerika Kaskazini hadi ghuba ya Meksiko[1].

Alitangazwa rasmi mwenyeheri na Papa Yohane Paulo II tarehe 22 Juni 1980, halafu mtakatifu na Papa Fransisko 3 Aprili 2014.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyofariki dunia[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.