Krisogoni (alifariki Aquileia, leo nchini Italia, 303 hivi) alikuwa mwanamume Mkristo wa Roma ya Kale ambaye aliuawa kwa sababu ya imani yake, inawezekana sana wakati wa dhuluma ya kaisari Dioklesyano[1].

Mt. Krisogoni akiwa amepanda farasi alivyochorwa na Michele Giambono (San Trovaso, Venice).

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Wa kwanza wanaadhimisha sikukuu yake tarehe 24 Novemba[2], wa pili tarehe 22 Desemba (pamoja na anayesemekana alikuwa mwanafunzi wake Anastasia wa Sirmio).

Katika Martyrologium Hieronymianum aliorodheshwa katika tarehe mbili tofauti: 31 Mei na 24 Novemba[3]

Krisogoni ni kati ya watakatifu wanaotajwa katika Kanuni ya Kirumi.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/90980
  2. Martyrologium Romanum, Libreria Editrice Vaticana (2001) ISBN 88-209-7210-7
  3. Martyrologia Hieronomianum, ed. De Rossi; Duchesne in Acta SS., Nov. II, cited in St. Chrysogonus from the Catholic Encyclopedia

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.