Liturujia ya Armenia

Liturujia ya Armenia ni liturujia maalumu ya Ukristo ambayo leo inatumiwa na Kanisa la Mitume la Armenia na vilevile na Kanisa Katoliki la Armenia kokote duniani.

Altare ya Kiarmenia ikiwa na ukuta wa picha takatifu na mapazia, Echmiatsin, Armenia.

Liturujia hiyo inafuata mapokeo ya Gregori Mletamwanga, mwanzilishi na msimamizi wa Kanisa huko Armenia.

Majengo hariri

Makanisa ya Kiarmenia kwa kawaida yana mapazia yanayotenganisha padri altareni na walei washiriki wakati wa sehemu fulanifulani za ibada, lakini si ukuta wa picha takatifu unaopatikana katika Makanisa ya Kiorthodoksi.

Athari za liturujia nyingine hariri

Daima liturujia hiyo imekuwa tayari kuathiriwa na madhehebu mengine. Kwa mfano, maaskofu wanavaa kichwani mitra kama wale wa Kanisa la Kilatini.

Pia unatumika mkate usiotiwa chachu kwa ajili ya ekaristi.

Kumbe ni jambo la pekee kutochanganya maji kidogo katika divai kama ilivyo desturi ya madhehebu mengine.

Kati ya anafora zote za Kiarmenia, kuanzia karne ya 10 inatumika ile tu inayoitwa ya Atanasi wa Aleksandria iliyotafsiriwa kutoka Kigiriki.

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Liturujia ya Armenia kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.