Waorthodoksi ni Wakristo wanaofuata mapokeo ya Mitume wa Yesu jinsi yalivyostawi kihistoria katika Ukristo wa Mashariki upande wa mashariki wa Dola la Roma iliyoitwa pia Bizanti na nje ya mipaka yake. Leo hii ni nchi za Ulaya ya Mashariki pamoja na nchi za Mashariki ya Kati ulipoenea baadaye dini ya Uislamu.

Maeneo ya Waorthodoksi katika Ulaya na Mashariki ya Kati
Asilimia ya Waorthodoksi duniani nchi kwa nchi:      Zaidi ya 75%      50–75%      20–50%      5–20%      1–5%      Chini ya 1%, lakini wenye haki ya kujitegemea

Jina hariri

Kanisa la Orthodoksi ni jina linalotumika hasa kumaanisha Kanisa la Kikristo linalokubali mamlaka ya kiroho ya mitaguso saba ya kiekumeni tu. Leo, hasa kwa sababu ya uhamiaji, Kanisa la Orthodoksi lipo katika dunia nzima, likijumuisha watu milioni 200 hivi, lakini bado lina idadi kubwa ya waumini katika Ulaya ya Mashariki.

Jina hilo ("Orthodoksi") lina asili ya Kigiriki likitokana na maneno όρθος ("orthos", yaani "nyofu", "sahihi") na δόξα ("doksa", yaani "rai", "fundisho") yaani "wenye fundisho sahihi".

Jina hilo lilitungwa ili kutofautisha Wakristo waliofuata mafundisho rasmi ya imani yaliyotolewa na Mitaguso ya kiekumene dhidi ya mikondo mingine ya wakati ule.

Kwa namna ya pekee jina hilo lilitumika upande wa mashariki, hivi kwamba lilipotokea farakano la mwaka 1054, likabaki kama jina maalumu la makanisa yenye ushirika na Patriarki wa Konstantinopoli (leo Istanbul katika Uturuki).

Muundo hariri

Makanisa ya kujitegemea ya Kiorthodoksi yanayotambuliwa na wote ni kama yafuatayo:

Makanisa mengine yaliyojitenga na hayo hayajakubalika.

Uhusiano na Waorthodoksi wa Mashariki na Wakatoliki wa Mashariki hariri

Hivi karibuni hata makanisa mengine ya mashariki yamechagua kujiita hivyo, ingawa yanaendelea kutofautiana kuhusu maazimio kadhaa ya mitaguso mikuu iliyokubaliwa na Wakristo walio wengi. Leo hii wanatofautisha kwa kutumia majina

  • "Waorthodoksi" kwa makanisa yaliyotokana na kanisa rasmi la Bizanti (Roma Mashariki) (kwa Kiingereza: Eastern Orthodox)
  • "Waorthodoksi wa Mashariki" kwa makanisa yaliyojitenga na kanisa hili la Bizanti (kwa Kiingereza: Oriental Orthodox)

Hata hivyo pande hizo mbili zinafanana katika teolojia, liturujia na staili za fahari za ibada zao, pia katika sheria kuhusu maaskofu (wasiooa), makasisi na mashemasi (wanaoweza kuwa watu wa ndoa), tena katika umuhimu wa umonaki na maisha ya kiroho.

Ni vilevile kuhusu Wakatoliki wa Mashariki ambao wana ushirika kamili na Papa wa Kanisa la Roma bila kuacha mapokeo ya Ukristo wa Mashariki.

Marejeo hariri

Vitabu hariri

Marejeo mengine hariri

Marejeo mengine tena hariri

  • Aderny, Walter F. The Greek and Eastern Churches (1908) online
  • Hussey, Joan Mervyn. The orthodox church in the Byzantine empire (Oxford University Press, 2010) online Archived 1 Agosti 2020 at the Wayback Machine.
  • Krindatch, Alexei D. ed., Atlas of American Orthodox Christian Churches (Holy Cross Orthodox Press, 2011) online.
  • Mascall, Eric Lionel (1958). "The Example of Orthodoxy", in his The Recovery of Unity: a Theological Approach (London: Longmans, Green, and Co.), p. 52-64. N.B.: Caption title; concerns especially the place and example of Eastern Orthodoxy in the Ecumenical Movement.
  • McGuckin, John Anthony, ed. (2011). The Encyclopedia of Eastern Orthodox Christianity. 2 vols. Wiley-Blackwell, Chichester, W. Sussex, UK. ISBN 978-1-4051-8539-4. 
  • Parry, Ken. ed., The Blackwell Companion to Eastern Christianity (2010); Comprehensive global coverage.
  • Stanley, Arthur Penrhyn (1869). Lectures on the History of the Eastern Church: with an Introduction on the Study of Ecclesiastical History. Fourth ed. London: J. Murray.

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Mahusiano na Kanisa Katoliki hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Waorthodoksi kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.