Maksimiliani wa Tebessa

Maksimiliani wa Tebessa (au Numidia; 274- 12 Machi 295) alikuwa kijana Mkristo katika Algeria ya leo aliyefia dini yake kwa kukatwa kichwa[1].

Mtoto wa askari Fabius Victor, alilazimishwa kujunga na jeshi la Dola la Roma, lakini alikataa kula kiapo cha uaminifu kwa Kaisari na kuwa mwanajeshi akitaja kama sababu imani yake[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 12 Machi[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Ott, Michael. "Maximilian." The Catholic Encyclopedia. Vol. 10. New York: Robert Appleton Company, 1911. 15 Mar. 2013
  2. Richard Alston, Soldier and Society in Roman Egypt, London and New York: Routledge, 1995, ISBN 0-415-12270-8, p 149.
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.