Malaika katika imani ya dini mbalimbali, kama vile Uyahudi, Ukristo na Uislamu, ni kiumbe wa kiroho tu anayeweza kutumwa na Mungu kwa binadamu.

Malaika wa uhuru.
Malaika aliyejeruhiwa, mchoro wa Hugo Simberg, 1903.

Kwa umbile lake hawezi kujulikana na hisi za mwili wetu.

Katika Biblia hawa tu wanatajwa kwa jina maalumu: malaika Mikaeli, malaika Gabrieli na malaika Rafaeli (huyo katika Deuterokanoni tu).

Katika Uislamu ni kiumbe chepesi ambacho kimeumbwa kwa nuru, nacho huwa hakanyagi chini kama mwanadamu, bali huelea juu au kuketi ndani ya moyo wa mwanadamu.

Katika Biblia hariri

Katika Biblia, malaika na watu ndio viumbe pekee vyenye hiari ya kuchagua wenyewe wachangie mpango wa Mungu au la. “Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi, chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako” (Kumb 30:19-20).

Malaika na watu wanaweza kuchagua hata wawe wema au wabaya milele. “Kulikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni” (Ufu 12:7-8). Chaguo letu binadamu linafanyika siku kwa siku kwa kuchukua misimamo mizuri au mipotovu kuhusu dini na maadili. “Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima” (Yoh 5:39-40).

Kati ya viumbe mbalimbali Mungu ameweka mpango: alitaka malaika wasioonekana wamtumikie kwa kutusaidia sisi watu, na vile vinavyoonekana tuvitumie kwa uadilifu ili kwa njia yetu vimtukuze yeye. “Atakuagizia malaika zake wakulinde katika njia zako zote” (Zab 91:11). “Kwa Hekima yako ulimwumba mwanadamu, ili avitawale viumbe vilivyoumbwa nawe, na kumiliki ulimwengu katika utakatifu na kwa haki” (Hek 9:2-3).

Malaika ni roho tupu walioumbwa na Mungu ili wamtukuze milele, wamlinde kila mtu na kumtumikia Bwana Yesu katika kutuokoa. “Angalieni, msidharau mmojawapo wadogo hawa, kwa maana nawaambia ya kwamba malaika zao mbinguni sikuzote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni” (Math 18:10).

  Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.