Mdudu mabawa-nusu
Kisulisuli mraba-mweusi (Dysdercus nigrofasciatus)
Kisulisuli mraba-mweusi (Dysdercus nigrofasciatus)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hemiptera (Wadudu wenye mabawa ya mbele yaliyo magumu kwa nusu tu)
Linnaeus, 1758
Ngazi za chini

Nusuoda 4:

Wadudu mabawa-nusu ni wadudu wadogo sana hadi wakubwa kiasi wa oda Hemiptera katika nusungeli Pterygota (wenye mabawa). Jina ni tafsiri ya jina la kisayansi. Wadudu hawa wanajulikana sana kama kunguni, kunguni-mgunda, vidukari, vidung'ata, nzi weupe, wadudu-gamba na nyenje-miti k.m. Familia kadhaa zina spishi zinazoishi majini, kama nge-maji, waogeleaji-juuchini na wendamaji. Spishi za Halobates huenda juu ya maji ya bahari na hizi ni wadudu pekee wanaoishi baharini.

Katika spishi nyingi sehemu ya mbele ya mabawa ya mbele ya wadudu hawa ni ngumu na sehemu ya nyuma ni kiwambo. Mabawa yakiwa yamekunjwa yanalala bapa na kufunika fumbatio. Mabawa ya nyuma ni kama viwambo. Katika spishi nyingine jozi zote mbili za mabawa ni kama viwambo na mara nyingi yakiwa yamekunjwa yanakaa kama paa la nyumba. Pengine mabawa yana manyoya (k.m. nzi weupe).

Sehemu za kinywa zinafaa kufyonza na zimeunda kwa mrija. Hufyonza utomvi wa mimea au damu ya wadudu wengine na hata ya mamalia katika spishi kadhaa. Spishi fulani za nusufamilia Triatominae zinaambukiza watu kwa ugonjwa wa Chagas, jamaa ya ugonjwa wa malale.

Wadudu hawa hutaga mayai juu ya majani au mashina ya mimea, lakini kuna spishi zinazozaa lava badala ya mayai, k.m. spishi nyingi za vidukari.

Spishi kadhaa za Afrika ya Mashariki hariri

Picha hariri