Mtumishi wa Mungu ni jina la heshima linalotumika katika Biblia na katika Ukristo kwa mtu anayesadikiwa kumtumikia Mungu kwa namna ya pekee.

Katika Biblia hariri

Katika Biblia ya Kiebrania ni la juu kuliko "nabii", kwa sababu jina hilo lilikuwa na maana mbalimbali, hata mbaya, kwa mfano "kichaa" au "nabii wa uongo".

Katika Ukristo hariri

Siku hizi linatumiwa na Wakristo wa madhehebu mbalimbali kwa maana tofauti.

Katika Kanisa Katoliki hariri

Katika Kanisa Katoliki linatumika hasa[1] kwa waumini wafu ambao maisha yao yameanza kuchunguzwa ili kuona kama hatimaye wataweza kutangazwa watakatifu.[2][3]

Jina Mtumishi wa Mungu halimaanishi kuwa kweli mhusika alimtumikia Mungu kiaminifu hadi kifo chake, bali kwamba watu wengiwengi wanaona hivyo, hata askofu wa jimbo alifungua kesi ya kumtangaza mtakatifu.

Baada ya hatua hiyo kukamilika kwa Papa kuthibitisha ushujaa wa maadili yake yote, au kifodini chake, mtumishi huyo ataanza kuitwa Mstahili heshima.

Kisha kuthibitisha kwamba muujiza wowote umetokea kwa maombezi yake, Papa atamtangaza mwenye heri.

Baada ya muujiza mwingine atamalizia kwa kumtangaza mtakatifu.[4][5]

Kesi hizo katika hatua zote zinasimamiwa na idara maalumu yenye makao makuu huko Vatikani.

Tofauti na hilo ni jina Servus Servorum Dei (Mtumishi wa mtumishi wa Mungu), ambalo kuanzia Papa Gregori I linatumiwa na Mapapa kujitambulisha.

Tanbihi hariri

  1. Congregatio de Causis Sanctorum – Vincenzo Criscuolo, Daniel Ols, Robert J. Sarno (ed.), Le Cause dei Santi. Sussidio per lo Studium, Libreria Editrice Vaticana, 3rd edition, Rome 2014, p. 342.
  2. "Pressing Sainthood for a Beloved Archbishop". (12 December 2004) by Marek Fuchs. The New York Times. Accessed 28 February 2010
  3. CONGREGATION FOR THE CAUSES OF SAINTS: NEW PROCEDURES IN THE RITE OF BEATIFICATION
  4. "John Paul II declared Venerable, moves one step closer to sainthood". CNA. Retrieved 28 February 2010
  5. Mercedarian Missionaries' founder to be beatified. Archived 8 Machi 2012 at the Wayback Machine. 5 October 2006. Saipan Tribune. Retrieved 28 February 2010
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtumishi wa Mungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.