Nguyễn Phú Trọng

Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Vietnam (kiongozi mkuu) tangu 2011

Nguyễn Phú Trọng (14 Aprili 1944 - 19 Julai 2024) alikuwa mwanasiasa wa Vietnam, kiongozi mkuu wa nchi tangu tarehe 19 Januari 2011 kama Katibu Mkuu wa sasa wa Chama cha Kikomunisti cha Vietnam. Tangu mwaka 2018 alikuwa pia Rais wa Vietnam, akiwa mtu wa tatu kuongoza kwa wakati mmoja chama na nchi baada ya Ho Chi Minh na Trường Chinh.

Picha yake.

Alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Kitaifa kutoka mwaka 2006 hadi 2011, akiwakilisha Hanoi. Alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Vietnam kwenye mkutano wa 11 wa Bunge la Kitaifa mnamo 2011 na kujadiliwa tena katika Mkutano wa 12 wa Kitaifa mnamo 2016.

Kama Katibu Mkuu, Trọng aliongoza Sekretarieti ya chama na kuwa Katibu wa Tume Kuu ya Jeshi pamoja na kuwa mkuu wa Politburo, chombo cha juu zaidi cha maamuzi nchini Vietnam, ambacho kilimfanya kuwa mtu mwenye nguvu zaidi huko Vietnam.

Mnamo Oktoba 3, 2018, Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha Vietnam ilimteua Trọng kuwa Rais ajaye wa Vietnam kupigwa kura kwenye kikao cha Bunge la Kitaifa ambapo chama hicho kinashikilia idadi kubwa. Basi, tarehe 23 Oktoba 2018, alichaguliwa kama Rais wa 9 wa Vietnam katika mkutano wa kikao cha sita cha Bunge la Kitaifa.

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nguyễn Phú Trọng kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.