Petro Shanel (Cuet, Ufaransa, 12 Julai 1803Futuna, Oseania, 28 Aprili 1841) alikuwa padri mmisionari wa Kanisa Katoliki.

Mt. Peter Chanel.

Ametambuliwa rasmi na Papa Leo XIII kuwa mwenye heri tarehe 17 Novemba 1889, halafu na Papa Pius XII kuwa mtakatifu kama mfiadini tarehe 12 Juni 1954.

Sikukuu yake ni tarehe 28 Aprili[1].

Maisha

hariri

Baada ya kupata upadrisho alishughulika na uchungaji nchini mwake kwa miaka michache, akiwajibika hasa kwa ajili ya wakulima na malezi ya vijana.

Halafu aliingia Shirika la Maria, akatumwa akatumwa katika visiwa vya Oceania pamoja na wenzake kadhaa kuhubiri Injili mahali ambapo ilikuwa haijatangazwa.

Licha ya matatizo mengi alifaulu kwa upole wake kuwaongoa watu kadhaa katika kisiwa cha Futuna, akiwemo mwana wa mfalme. Kwa sababu ya kuchukiwa kwa imani ya Ukristo, huyo kwa hasira aliagiza akamatwe na kuuawa kwa kupigwa rungu [2].

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri
  1. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/26950

Marejeo ya Kiswahili

hariri
  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 147-148
  • Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 126-127
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.