Sesari wa Nazianzo

Sesari wa Nazianzo (Arianzo, leo Güzelyurt, mkoani Kapadokia, katikati ya nchi ambayo leo inaitwa Uturuki, 331 hivi - Nazianzo, 369 hivi) alikuwa mganga wa ikulu[1][2][3].

Picha takatifu ya Mt. Sesari.

Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[4].

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 25 Februari[5].

Maisha hariri

Alizaliwa katika familia ya kisharifu ya watakatifu. Baba yake aliitwa Gregori mzee na mama yake Nonna. Kaka yake alikuwa Gregori wa Nazienzi.

Baba, aliyekuwa Myahudi, aliongokea Ukristo kwa msaada wa mke wake na hatimaye akawa askofu wa Nazianzo.

Hata hivyo Sesari alibatizwa tu muda mfupi kabla hajafa kwa tauni, baada ya kunusurika kufa katika tetemeko la ardhi lililopata mji wa Nisea alipokuwa afisa wa serikali.

Alikuwa amesoma fani mbalimbali kwanza huko Kaisarea wa Kapadokia, halafu Aleksandria ya Misri, alipowazidi wanafunzi wenzake wote[6].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Monks of Ramsgate. “Caesarius of Nazianzum”. Book of Saints, 1921. CatholicSaints.Info. 19 September 2012
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/42650
  3. Caesarius was the main character in a historical novel Gods and Legions, by Michael Curtis Ford (2002). The novel, which tells the story of the rise and fall of Julian the Apostate, is narrated by Caesarius who is, according to the story, his closest companion.
  4. Rosemary Guiley (2001). The Encyclopedia of Saints. Infobase Publishing. pp. 60–. ISBN 978-1-4381-3026-2. 
  5. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
  6. Weber, Nicholas. "St. Caesarius of Nazianzus." The Catholic Encyclopedia. Vol. 3. New York: Robert Appleton Company, 1908. 8 Mar. 2014

Vyanzo hariri

  • McGuckin, John A. St. Gregory of Nazianzus: An Intellectual Biography. Crestwood, NY: 2001, St. Vladimir's Seminar Press. ISBN|0-88141-222-8
  • Migne, J.P. (General Editor). Cursus Completus Patrologiae Graecae. 167 volumes. Paris: 1857-1866.
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.