Stefano wa Perm (kwa Kirusi Стефан Пермский; 26 Aprili 1340 - 26 Aprili 1396[1]) alikuwa mmonaki mchoraji aliyeleta Ukristo kwa Wakomi na kuwa askofu wa kwanza wa jimbo la Perm, akibomoa sanamu za miungu na kujenga makanisa, mbali na kubuni mwandiko wa Kiperm na kutumia lugha ya wenyeji katika kuthibitisha imani na kuadhimisha liturujia[2].

Picha takatifu ya Mt. Stefano njiani kuelekea Moscow.
Alivyochora fumbo la Utatu.

Alitangazwa na Kanisa la Kiorthodoksi la Urusi kuwa mtakatifu tarehe 26 Aprili 1754. Anaheshimiwa hivyo na Kanisa Katoliki pia.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Aprili[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Janet Martin, Medieval Russia, 980-1584, (Cambridge, 1995), p. 225
  2. Serge A. Zenkovsky, Medieval Russia's Epics, Chronicles, and Tales, Revised Edition, (New York, 1974), p. 259
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • Ferguson, Charles. 1971. St. Stefan of Perm and applied linguistics. (Originally published in 1967, in To Honor Roman Jakobson, ed. by Morris Halle, pp. 643–653. The Hague: Mouton. Also reprinted in 1968 Language Problems of Developing Nations, ed. by Joshua Fishman, Charles Ferguson, and J. Das Gupta, pp. 27–35. New York Wiley and Sons.) Language Structure and Language Use: Essays by Charles Ferguson, ed. by Answar S. Dil, pp. 197–218. Stanford: Stanford University Press.
  • Martin, Janet, Medieval Russia, 980-1584, (Cambridge, 1995), pp. 225–6
  • Zenkovsky, Serge A. (ed.), Medieval Russia's Epics, Chronicles, and Tales, Revised Edition, (New York, 1974), pp. 259–62

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.