Sultani al-Hasan ibn Sulaiman

Sultani al-Hasan ibn Sulaiman (kwa Kiarabu: الحسن بن سليمان), mara nyingi hujulikana kama "Abu'l-Muwahib" ("baba wa zawadi"), alikuwa mtawala wa Kiarabu katika kisiwa cha Kilwa, kinachopatikana Tanzania ya sasa; alitawala tangu mwaka 1310 hadi 1333. Jina lake kamili lilikuwa Abu al-Muzaffar Hasan Abu al-Muwahib bin Sulaiman al-Mat'un bin Hasan bin Talut al-Mahdal.

Historia hariri

Al-Hasan ibn Sulaiman alikuwa mwanachama mwenye vinasaba vya Mahdali, na alisimamia katika kipindi cha ustawi wa mji mkuu wa Kilwa.

Mahdal wanadai vinasaba vya sultani vilikuwa ni Uislamu. Alijenga Ikilu ya Husuni nje ya mji na kufanya upanuzi mkubwa wa Msikiti Mkuu wa Kilwa.

Ujenzi huo inaonekana ulichagizwa na Hija ya sultani huko Makka, ambaye alitaka kuiga majengo yale makubwa. Mwaka 1331 Ibn Battuta alitembelea mahakama ya Sultani na kuelezea ukarimu wake. Ndiyo chanzo cha jina la "baba wa zawadi".

Marejeo hariri