Wamanyema (Una-Ma-Nyema, yaani Wala-samaki), ni shirikisho la makabila 12 ya Kibantu yanayopatikana kusini mashariki mwa beseni la mto Kongo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na katika mkoa wa Kigoma nchini Tanzania.

Kijiji cha Wamanyema 1876

(Manyema Association) imeundwa miaka ya 1930, na inajumuisha makabila 18 ya Wamanyema yaliyounganishwa kwa imani ya dini ya Kiislamu na asili ya kuhama mashariki mwa Kongo ya Kibelgiji au Kongo ya Kiarabu.

Kwa Tanzania, wanajumuisha makabila ya Wagoma, Wabwari, Wamasanze, Wabembe, Waholoholo n.k. ambao wote hujiita Wamanyema.

Kwa sehemu kubwa ya karne ya 19 waliwindwa sana na Waarabu waliofanya biashara ya watumwa.

Wamanyema walipofika Kigoma kuna ambao walipata majina katika miji kama Katonga, Kabwe, Mkabogo au Kabogo: hao wote walikuwa Wamanyema wenye asili ya Kongo.

Inafahamika kuwa Waha ni moja ya makabila kutoka Wabantu wa mashariki. Wabantu hao walipata kufika maeneo hayo hata kabla ya miaka ya 600 yaani kabla ya Wamanyema. Waha waliwapokea watani wao Wamanyema na kuanza kuishi pamoja mpaka sasa.

Hivyo Wamanyema na Waha ndio wenyeji wa Kigoma. Uenyeji huu tunaouzungumza ni miaka ya zamani sana: hata kabla ya kuanza kwa ukoloni hawa watu tayari walikuwa wakiishi pamoja na walikuwa wakipendana na kuthaminiana. Kuna vitu Waha waliwafundisha Wamanyema na pia kuna vitu Wamanyema waliwafundisha Waha na wote hawa waliipigania Tanganyika kutoka mikononi mwa serikali ya kikoloni. Hata mradi wa kuligawa bara la Afrika kati ya nchi kadhaa za Ulaya ulikuwa bado kabisa Wamanyema na Waha walikuwa wakiishi pamoja.

Watu maarufu hariri

Makala yenye habari za kimdomo bila vyanzo halisi

Makala hii (au sehemu zake) inaonekana kutoa habari za kimdomo kuhusu desturi au utamaduni wa maeneo ya Tanzania. Hailingani na masharti ya kuonyesha vyanzo na ushuhuda wa kimaandishi jinsi ilivyo kawaida katika Wikipedia.

Lakini ilhali habari nyingi katika mazingira yetu hazikuandikwa bado wala kujadiliwa kimaandishi na wataalamu tunaacha habari hizi kwa muda. Tunaomba wasomaji wetu kuwa macho na kutochanganya habari hizi za kisimulizi na habari zenye ushuhuda halisi. Tunaendelea kuangalia michango ya aina hii ambayo haiwezi kukubaliwa jinsi ilivyoletwa kama inapingana na ushuhuda halisi..

  Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wamanyema kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.