Warshawa

(Elekezwa kutoka Warsaw)






Warshawa (kwa Kipoland: Warszawa; kwa Kiingereza Warsaw) ni mji mkuu wa Poland pia mji mkubwa wa nchi, wenye wakazi milioni mbili hivi (1.78 mln - 2018).

Warshawa
Kitovu cha kihistoria cha Warshawa
Kitovu cha kihistoria cha Warshawa
Kitovu cha kihistoria cha Warshawa

Bendera

Nembo
Warshawa is located in Poland
Warshawa
Warshawa

Mahali pa Warshawa katika Earth

Majiranukta: 52°14′00″N 21°01′00″E / 52.23333°N 21.01667°E / 52.23333; 21.01667
Nchi Poland
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 1 729 119 (30.06.2014)
Tovuti:  http://www.um.warszawa.pl/

Jiografia

hariri

Warshawa iko katikati ya bonde la mto Vistula (Kipoland: polnisch Wisła, takriban km 350 kutoka Bahari Baltiki.

Historia

hariri

Warshawa imekuwa mji tangu karne ya 13, ikawa mji mkuu wa Poland mwaka 1596.

Iliharibiwa mara nyingi katika historia yake, hasa wakati wa vita kuu ya pili ya dunia. Wapoland walijaribu kuasi dhidi ya Wajerumani walioshika mji kati ya miaka 1939 na 1944; pamoja na vifo vingi, asilimia 90 za nyumba zote ziliharibiwa.

Baada ya vita mji ulijengwa upya mara nyingi kwa kurudisha nyumba zinazofanana na nyumba za kale.

Kitovu chake kimeorodheshwa na UNESCO kati ya mahali pa Urithi wa Dunia.

Utamaduni

hariri

Kuna vyuo 66 pamoja na Chuo Kikuu cha Warshawa, vyuo vikuu vingine, nyumba za maigizo, opera na makumbusho mbalimbali.

Uchumi

hariri

Warshawa ni mji wa viwanda vingi vya kutengenezea chuma, mashine, motokaa na mengine mengi.

Picha za Warshawa

hariri

Tazama pia

hariri

Viungo vya nje

hariri
 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu maeneo ya Poland bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Warshawa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.