Yohane Grande Román, O.H. (aliyependa kuitwa Yohane Mkosefu; Carmona, 6 Machi 1546 - Jerez de la Frontera, 3 Juni 1600) alikuwa bradha wa shirika la kihospitali la Mt. Yohane wa Mungu nchini Hispania.

Sanamu yake.

Kabla ya hapo alikuwa ameanzisha hospitali mwenyewe, ila aliamua kuiunga na shirika hilo mwaka 1574.

Aling'aa kwa upendo kwa wafungwa na waliotengwa na jamii: alipokuwa anahudumia wagonjwa wa tauni aliambukizwa akafa[1][2].

Papa Pius IX alimtangaza kwanza mwenye heri tarehe 13 Novemba 1858, halafu Yohane Paulo II akamtangaza mtakatifu tarehe 2 Juni 1992[3] [4].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[5].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. "Juan Grande Román (1546-1600)". The Holy See. Iliwekwa mnamo 22 May 2015.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. "Saint John Grande". Saints SQPN. 22 May 2009. Iliwekwa mnamo 22 May 2015.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  3. "Saint John Grande". Saints SQPN. 22 May 2009. Iliwekwa mnamo 22 May 2015.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  4. "Juan Grande Román (1546-1600)". The Holy See. Iliwekwa mnamo 22 May 2015.  Check date values in: |accessdate= (help)
  5. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.