Yosefu Zhang Dapeng

Yosefu Zhang Dapeng (Duyun, 1754 hivi - Guiyang 12 Machi 1815) alikuwa mlei katekista wa China aliyefia Ukristo kwa kusulubiwa.

Wafiadini Wakatoliki wa China.

Alipopokea mwanga wa imani, mara baada ya kubatizwa aliwafungulia nyumba yake wamisionari na makatekista akasaidia kwa kila namna watu fukara, wagonjwa na watoto. Alipopelekwa kwenye mateso ya msalabani, alimwaga machozi ya furaha kwa kujaliwa neema ya kumfia Yesu.

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu pamoja na wengine 119 tarehe 1 Oktoba 2000.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 9 Julai, lakini ya kwake mwenyewe tarehe 12 Machi[1].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.