Abdallah Possi

Balozi

Dk. Abdallah Saleh Possi (amezaliwa 25 Agosti 1979) ni balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani. Amekubaliwa pia kama balozi huko Austria, Bulgaria, Ucheki, Ukulu mtakatifu, Hungaria, Poland, Romania na Uswisi. [1]

Dr Abdallah Saleh Possi


Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani
mtangulizi Philip Sang'ka Marmo

tarehe ya kuzaliwa 25 Agosti 1979 (1979-08-25) (umri 44)
Dar es Salaam, Tanzania
utaifa Mtanzania
mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (LL.B., LL.M.)
Chuo Kikuu cha Erlangen–Nuremberg (Uzamivu)

Kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi, Dk Possi aliwahi kuwa mbunge wa chama cha kisiasa cha CCM kwa uteuzi wa rais kwa miaka 20152020, tena naibu waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu. [2]

Hapo awali, alifanya kazi kama mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dodoma nchini Tanzania. Alikuwa pia wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na mkufunzi katika Taasisi ya Tawala za Mahakama huko Lushoto, Tanga, Tanzania.

Ana LL. B. na LL. M. kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na shahada ya uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Erlangen-Nuremberg huko Ujerumani.

Vitabu vyake hariri

  • POSSI, A. (2018) ‘Integrating Persons with Disabilities in the East African Labour Market A Comparative Analysis of Employment and Disability Laws in Tanzania, Kenya and Uganda’, in J. DÖVELING et al. (eds), Harmonisation of Laws in the East African Community: the State of Affairs with Comparative Insights from the European Union and other Regional Economic Communities, 5 TGCL Series, 213–242.
  • POSSI, A. & POSSI, A. ‘The identity Question versus Appropriateness of legal Anti-discrimination Measures: Endorsing the Disability Rights Approach to Albinism’, African Disability Rights Yearbook, 5 (2017), 118 -140. http://www.adry.up.ac.za/index.php/section-a-articles-2017/abdallah-possi-ally-possi Archived 21 Juni 2020 at the Wayback Machine.
  • POSSI, A. ‘Implementing Article 33 of the CRPD: Tanzanian approach’, African Disability Rights Yearbook, 4 (2016), 191–210. http://www.adry.up.ac.za/index.php/section-a-articles-4-2016/abdallah-possi Archived 22 Juni 2020 at the Wayback Machine.
  • POSSI, A. ‘Relating Equality and Disability Approaches in Tanzania: The Law in Tanzania Mainland and Zanzibar’, Zanzibar Yearbook of Law, 5 (2015), 3 – 29. http://www.zlsc.or.tz/documents/VOLUME%205.pdf Archived 8 Oktoba 2018 at the Wayback Machine.
  • POSSI, A. ‘Criminal Justice in Disrepute: An Overview of Treatment of Accused Persons and Convicts in Tanzania’, The Open University Law Journal, 1/1 (2007), 83–97. huo Kikuu Huria, 1/1 (2007), 83-97.

Marejeo hariri

  1. https://de.tzembassy.go.tz
  2. Makoye, Kizito. "Tanzania appoints first albino deputy minister", Deutsche Welle, 2015-12-15. 

Viungo vya nje hariri

Mabalozi wa Tanzania