Fransisko Maria wa Camporosso
Fransisko Maria wa Camporosso, O.F.M.Cap. (Camporosso 1804 - Genova 1866) alikuwa mtawa ombaomba wa shirika la Ndugu Wadogo Wakapuchini kutoka mkoa wa Liguria nchini Italia.
Alipata umaarufu mjini Genova kwa upendo wake katika kuombaomba mitaani kwa ajili ya shirika lake na ya mafukara aliowatembelea na kuwaombea.
Hatimaye alijitoa mhanga ili kipindupindu mjini kikome ikawa hivyo.
Alitangazwa na Papa Pius XI kuwa mwenye heri tarehe 30 Juni 1929, halafu Papa Yohane XXIII akamtangaza mtakatifu tarehe 9 Desemba 1962.
Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 17 Septemba[1].
Tazama pia Edit
Tanbihi Edit
Viungo vya nje Edit
- Tovuti ya kimataifa ya Ndugu Wakapuchini Archived 2 Aprili 2013 at the Wayback Machine.
- ORDO FRATRUM MINORUM — OFM — Tovuti ya Wafransiskani OFM
- Franciscans International
- Ndugu Wafransisko Wakapuchini
- Habari kwa Kiitalia Archived 21 Septemba 2008 at the Wayback Machine.
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |