Hanani (kwa Kiebrania חנני, Ḥănānî, maana yake: "YHWH amefadhili"; alizaliwa karne ya 10 KK) alikuwa nabii nchini Israeli katika karne ya 9 KK.

Alikuwa baba wa nabii Yehu na inafikiriwa kwamba waliishi kusini[1] .

Chanzo kikuu cha historia yake ni Kitabu cha pili cha Mambo ya Nyakati, sura ya 16[2] .

Kadiri ya kitabu hicho, alimlaumu mfalme wa Yuda Asa kwa kufanya agano na mfalme wa Shamu Ben-Hadad I. Kwa ajili hiyo alifungwa na Asa bila kujali malalamiko ya wafuasi wa nabii huyo.

Wengineo hariri

Katika Biblia ya Kiebrania kuna watu wengine watatu wenye jina hilohilo:

Tanbihi hariri

  1. Exell, J. and Spence-Jones, H. (eds.), Pulpit Commentary on 1 Kings 16, accessed 27 October 2017
  2. Barnes, W. E. (1899), Cambridge Bible for Schools and Colleges on 2 Chronicles 16, accessed 2 May 2020

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Hanani kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.