Irene Pancras Uwoya (alizaliwa 18 Desemba 1988) ni mwigizaji na mwongozaji wa filamu, mwanamitindo wa zamani na mjasiriamali kutoka nchini Tanzania. Irene pia alishiriki mashindano ya "Miss Tanzania" na kushika nafasi ya tano mwaka 2006/2007 [1][2]

Irene Pancras Uwoya
Amezaliwa 18 Desemba 1988 (1988-12-18) (umri 35)
Dodoma, Tanzania
Jina lingine Oprah
Kazi yake Mwigizaji
Mwanamitindo
Miaka ya kazi 2007
Ndoa Cyprus Hamad (mtalaka), Dogo Janja (mtalaka)
Watoto 1
Tovuti rasmi

Alifahamika sana kwa uhusika wa "Oprah" (2008) alioshiriki na Steven Kanumba na Vincent Kigosi. Baadhi ya filamu alizocheza ni pamoja na Uliyemchokoza Kaja, Figo, Rosemary, Snitch, The Return of Omega na Money.

Uwoya alianza shule ya msingi Mlimwa kisha akahamia Shule ya Bunge iliyopo Dar-es-Salaam kwa ajili ya elimu ya upili. Baadaye akaenda Greenville jijini Kampala, Uganda.[3][4]

Kwenye mwezi Oktoba 2017, habari zilitapakaa katika mitandao mbalimbali nchini Tanzania kuwa Uwoya ameolewa na Dogo Janja - msanii wa hip-hop Tanzania.[5] Siku kadhaa mbele kupitia ukurasa wake wa Instagram Uwoya alithibitisha kuolewa na Dogo Janja.[6]

Baadhi ya filamu zake hariri

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2023-09-25. Iliwekwa mnamo 2017-09-15. 
  2. Douglas Mwarua (2019-10-25). "TZ actress Irene Uwoya breaks down on live TV narrating struggles as single mum". Tuko.co.ke - Kenya news. (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2023-05-14. 
  3. Irene Uwoya katika Mybiohub.
  4. Irene Uwoya Archived 25 Septemba 2023 at the Wayback Machine. katika Bongo Cinema.com
  5. Irene Uwoya na Dogo Janja wafunga ndoa? Bongo5, October 29, 2017.
  6. Irene Uwoya afunguka kuolewa na Dogo Janja EATV mnamo MONDAY , 30TH OCT , 2017.
  Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Irene Uwoya kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.