Lilith ni jina la mwanamke ambaye katika hadithi fulani za Mesopotamia ya kale anatajwa kama mungu mke ambaye anahusika na dhoruba akazaa majini.

[[:Picha:]]==Katika Biblia== Biblia inasimulia jinsi dunia ilivyoumbwa na mwanzo wa binadamu. Katika maandiko hayo, masimulizi ya uumbaji yana changamoto kuyafahamu sawasawa, hususani kitabu cha Mwanzo 1:26 na Mwanzo 2. Uumbaji wa mwanamke unatajwa sehemu hizo mbili, lakini kwa namna tofauti, kwa kuwa ni visasili tofauti. Katika Mwa 1:26 Mungu aliwaumba Adamu na Eva sawia kwa sura na mfano wake. Katika Mwa 2 Mungu anamuumba Hawa baada ya kuchukua ubavu wa Adamu na kumfanya mwanamke.

Katika Biblia Isa 34:14 tu inamtaja Lilith, na jina hilo linatafsiriwa pengine "Bundi", sambamba na wanyama wengine saba wanaotajwa katika mstari huohuo na ule unaofuata.

Hata hivyo kuanzia karne ya 10 BK wametokea watu wanaodai Lilith, si Hawa, ndiye mwanamke wa kwanza ulimwenguni naye aliumbwa na Mungu wakati mmoja na Adamu. Wanasema Lilith alifukuzwa na kukataliwa na Mungu baada ya kupatikana kuwa mwenye nguvu zaidi na mwenye akili zaidi ya Adamu na hakutii amri za Adamu.

Wanadai Lilith haitajwi katika kitabu cha Mwanzo kwa kuwa inakwenda kinyume na jadi ya kutaka mnanamke atii mwanamume na wanawake kuwa katika hali ya chini kuliko wanaume. Wanadai pia Biblia ya sasa imepitia vichujio vingi vya kidini ili kuhakikisha kwamba inapoteza baadhi ya sehemu muhimu. Hata hivyo, kuna sehemu ambayo imeachwa ndani yake (Mwa 1) ambayo inaonyesha kwamba Mungu hakumuumba mwanamume tu bali alimuumba mwanamke kwa wakati huohuo, badala ya simulizi la ubavu kuchukuliwa kutoka kwa Adamu kama ilivyopendekezwa kwenye sura ya 2.

Jibu la msingi la Wayahudi na Wakristo ni kwamba imani inawadai kupokea Biblia kama ilivyo sasa, si katika hatua za awali ambazo tena ni za kufikirika tu.

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.