Marana na Sira (walifariki 450 hivi) walikuwa mabikira wa Berea, leo Aleppo, Syria, walioishi maisha magumu sana na kimya cha karibu mfululizo katika banda lisilowakinga dhidi ya hali ya hewa, wakitegemea chakula kutoka kwa wahisani waliotembelea makazi yao na kuwapa dirishani.

Theodoreto wa Kuro aliandika juu yao sura XXIX ya kitabu chake "Religiosa Historia" walipokuwa bado hai.

Tangu kale wanaheshimiwa kama watakatifu mabikira.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 28 Februari[1].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.