Papa Theodor I alikuwa Papa kuanzia tarehe 12 Oktoba/24 Novemba 642 hadi kifo chake tarehe 14 Mei 649[1]. Mzaliwa wa Yerusalemu (Israeli)[2] ambapo baba yake alipata kuwa askofu [3], alikimbilia Roma Waislamu walipoteka Nchi Takatifu[4].

Papa Theodori I.

Alimfuata Papa Yohane IV akafuatwa na Papa Martin I.

Alipinga uzushi wa waliokanusha Yesu kuwa na utashi wa kibinadamu na kwa ajili hiyo aliandaa Mtaguso wa Laterano wa mwaka 649 akishirikiana na Maksimo Muungamadini.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 18 Mei.[5]

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  3. Anastasius (bibliothecarius) (1602). Bibliothecarii Historia, de vitis romanorvm pontificvm. in typographeio I. Albini. p. 67. Theodorus, natione Grecus, ex patre Theodoro episcopo de civitate Hierusolima 
  4. Paul F. Bradshaw (2013). New SCM Dictionary of Liturgy and Worship. Hymns Ancient and Modern Ltd. p. 5. ISBN 9780334049326. 
  5. Ὁ Ἅγιος Θεόδωρος ὁ Ἱερομάρτυρας Ἐπίσκοπος Ρώμης. 18 Μαΐου. ΜΕΓΑΣ ΣΥΝΑΞΑΡΙΣΤΗΣ.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Theodor I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.