Raga
Raga (ing. rugby) ni jina la mchezo wa mpira unaochezewa kwa namna mbalimbali.

Rugby ilianzishwa nchini Uingereza sambamba na mpira wa miguu Wakati wa karne ya 19. American Football imezaliwa kutoka kwa rugby ya Kiingereza.
Shabaha ya mchezo ni kubeba au kukanyaga mpira kupitia timu ya wapinzani hadi goli na kuuingiza kwenye goli juu ya mti wa kulala.
Mpira una umbo la duaradufu. Timu mbili ambazo kwa kawaida huwa na wachezaji 15 zinashindana. Mpira unaweza kushikwa kwa mkono; kuna rukhsa kuupa kwa mchezaji mwingine au kuutupa nyuma. Lakini kuutupa mbele ni kosa ndogo unaofuatwa na tendo la "scrum". Hapo mpira unawekwa chini na wachezaji 8 wa kila timu wanashikamana na kusukumana hadi mchezaji mmoja anaweza kushika tena mpira.
Kuna rukhsa kumzuia mchezaji na kumwangusha kwa kumshika nyuma ya msari wa mabega. Tendo hili linaitwa "tackle". Akianguka china anapaswa kuachana na mpira. Wakati mchezaji analala chini wengine hawaruhusiwi kushika mpira kwa mikono.
-
Scrum
-
Mpira wa rugby
-
Goli
-
Tackle
-
Timu ya rugby ya Cote d'Ivoire