Georgia
Kwa matumizi mengine ya jina hili tazama Georgia (maana) Georgia ni nchi iliyoko kati ya Ulaya ya Mashariki na Asia ya Magharibi. Ni sehemu ya eneo la Kaukazi, ikipakana na Bahari Nyeusi upande wa magharibi, Urusi upande wa kaskazini na kaskazini-mashariki, Uturuki upande wa kusini-magharibi, Armenia upande wa kusini, na Azerbaijan upande wa kusini-mashariki.
Georgia საქართველო (geo)
|
||||||
---|---|---|---|---|---|---|
|
||||||
Wito: ძალა ერთობაშია(Kigeorgia) "Nguvu ni Umoja" |
||||||
Wimbo wa taifa: Tavisupleba ("Uhuru") | ||||||
![]() Eneo la Georgia katika ramani ya Dunia
|
||||||
Mji Mkuu and largest city | Tbilisi 41°43′N 44°47′E / 41.717°N 44.783°E | |||||
Official languages | Kigeorgia (pia Kiabkhazi katika Abkhazia) | |||||
Government | Jamhuri | |||||
Chanzo cha Taifa | ||||||
Idadi ya watu | ||||||
- | 2017 Makisio | 3,718,200[1] (ya 1311) | ||||
- | 2014 Sensa | 3,729,635 | ||||
Pato la Taifa PPP | ||||||
- | Jumla | $35.91 | ||||
- | Per capita | $3,400 | ||||
HDI (2022) | 0.814 very high ·60th |
|||||
Currency | Lari (ლ) (GEL ) |
|||||
Saa za eneo | Moscow Time (MSK) (UTC+3) | |||||
- | Summer (DST) | Moscow Summer Time (MSD) (UTC+4) | ||||
Calling code | 995 | |||||
Patron saint | Mt. George, Bikira Mariamu | |||||
Internet TLD | .ge | |||||
1 Population figure excludes Abkhazia and South Ossetia. |
Georgia inachukua eneo la kilomita za mraba 69,700 (maili za mraba 26,900). Ina idadi ya watu milioni 3.7, ambapo zaidi ya theluthi moja wanaishi katika mji mkuu na mji mkubwa zaidi, Tbilisi. Wenyeji wa Georgia, ambao ni asili ya eneo hilo, wanaunda sehemu kubwa ya idadi ya watu wa nchi hiyo na ndio taifa kuu.
Jiografia
haririGeorgia ni nchi ya milima inayofikia kimo cha mita 5,068. Kati ya safu mbili za milima kuna tambarare ya Kolkhis.
Upande wa magharibi unafaidika zaidi na Bahari Nyeusi, hivyo una hali ya hewa safi na mvua nyingi inayofaa kwa kilimo hasa cha mizabibu.
Historia
haririGeorgia ilikuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti lakini imekuwa nchi huru tangu 1991.
Maeneo ya Abkhazia na Ossetia ya Kusini yamedai uhuru pia na kwa sasa hayapo chini ya serikali kuu, lakini hayatambuliki kimataifa.
Utamaduni
haririWakazi walio wengi (71%) huzungumza lugha ya Kigeorgia lakini kuna vikundi vya wazungumzaji wa Kirusi (9%), Kiarmenia (7%), Kiazeri (6%) na lugha nyingine.
Wageorgia wengi ni Wakristo wanaofuata Kanisa la Kiorthodoksi la Georgia (83.9%). Kuna pia wafuasi wa Kanisa la Kitume la Armenia (3.9%) na Wakatoliki (0.8%). Waislamu ni 9.9%, wakati Wayahudi wanazidi kuhama.
Watu maarufu
haririMgeorgia anayejulikana zaidi duniani alikuwa Josef Stalin, mtawala wa Urusi wakati wa Ukomunisti.
Tazama pia
haririTanbihi
hariri- ↑ "Number of Population as of January 1, 2017 — National Statistics Office of Georgia" (PDF). Retrieved 1 May 2017.
Viungo vya nje
hariri- Serikali
- President of Georgia Ilihifadhiwa 7 Aprili 2013 kwenye Wayback Machine.
- Government of Georgia Ilihifadhiwa 27 Aprili 2011 kwenye Wayback Machine.
- Ministry of Foreign Affairs of Georgia Ilihifadhiwa 4 Mei 2011 kwenye Wayback Machine.
- Department of Tourism and Resorts Ilihifadhiwa 5 Januari 2009 kwenye Wayback Machine.
- American Chamber of Commerce in Georgia
- Chief of State and Cabinet Members Ilihifadhiwa 24 Juni 2013 kwenye Wayback Machine.
- Taarifa za jumla
- Georgia entry at The World Factbook
- Georgia Ilihifadhiwa 7 Juni 2008 kwenye Wayback Machine. at UCB Libraries GovPubs
- Georgia katika Open Directory Project
- Georgia profile from the BBC News
- Wikimedia Atlas of Georgia
- Association of Modern Scientific Investigation – (AMSI)
- News media
- Civil Georgia, daily news about Georgia
- Crisis profile, Georgia, Abkhazia, S. Ossetia Ilihifadhiwa 10 Juni 2009 kwenye Wayback Machine. From Reuters Alertnet Ilihifadhiwa 11 Machi 2009 kwenye Wayback Machine.
- Georgian Daily Ilihifadhiwa 17 Oktoba 2008 kwenye Wayback Machine., all the latest news from Georgia and related to Georgia
- NewsGeorgia Google Translation into English from the NewsGeorgia (Russian Language) site
- GeorgiaCaucasus.com GeorgiaCaucasus.com – online info Magazine dedicated to Georgia and Caucasus
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Georgia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Georgia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |