Roko, Alfonso na Yohane

Roko, Alfonso na Yohane (walifariki Caaró, leo nchini Brazil, 15 Novemba na 17 Novemba 1628) walikuwa mapadri wa shirika la Yesu ambao walifia imani ya Kikristo wakifanya umisionari kati ya Waindio.

Wafiadini wote watatu. Mt. Yohane wa Castillo uko upande wa kulia.
Mt. Roko Gonzalez.
Sanamu ya Mt. Alfonso Rodriguez-Olmedo.

Alfonso na Yohane walitokea Hispania, kumbe Roko alizaliwa Asuncion, katika Paraguay ya leo.

Wanaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama watakatifu wafiadini. Kwanza walitangazwa na Papa Pius XI kuwa wenye heri tarehe 28 Januari 1934, halafu watakatifu na Papa Yohane Paulo II tarehe 16 Mei 1988.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 15 Novemba [1].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Clement J. McNaspy, S.J.: Conquistador without Sword. The Life of Roque González, S.J., Chicago, Loyola University Press, 1984, 206pp.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.