Roma (maana)

ukarasa wa maana wa Wikimedia

Roma (pia: Rumi) ni jina linalotumika kwa mji wa Roma (mji mkuu wa Italia), ama kwa dola la Roma lililokuwa kwa karne kadhaa kabla na baada ya Kristo dola kubwa kuliko zote duniani, tena kwa Kanisa la Roma ambalo ni kiini cha Kanisa Katoliki lote. Lilikuwa pia jina la mungu wa kike katika dini ya Roma ya Kale.

Roma 2017

Roma au Rumi? hariri

Roma ni umbo asili la jina katika Kilatini na Kiitalia; limekuwa pia la kawaida katika Kiswahili cha kisasa.

Kumbe "Rumi" ilikuwa kawaida katika Kiswahili cha zamani kutokana na kawaida ya lugha ya Kiarabu (الرُّومُ ar-Rūm).

Matoleo ya Biblia ya "Union Version" iliyochapishwa tangu 1952 hutumia "Rumi", "Warumi". Kumbe tafsiri ya Biblia ya "Kiswahili cha Kisasa" hutumia "Roma", "Waroma".

Historia hariri

21 Aprili 753 KK ndiyo tarehe ya kimapokeo ambayo mji huo ulisemekana kuundwa na mapacha Romulo na Remo. Ukweli ni kwamba ulianzishwa mapema zaidi (1000 K.K. hivi).

 
Ukurasa huu una maelezo ya maana ili kutofautisha nia mbalimbali zinazolengwa na neno moja. Kwa usaidizi kuhusu makala za aina hii tazama Msaada:Maana

Maelezo katika ukurasa huu yawe mafupi, na kwa kila maana kuwe na kiungo kimoja tu ambacho kiunge ukurasa kuhusu nia yenye maana hii. Ukiwa umefika hapa kwa kutumia kiungo katika makala nyingine, tafadhali badalisha kiungo kile kiunge makala iliyokusudiwa moja kwa moja.