Masokwe
(Elekezwa kutoka Sokwe (Hominoidea))
Sokwe | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||
Familia 2:
|
Masokwe (wingi wa sokwe) ni wanyama wa familia ya juu Hominoidea.
Kuna familia mbili za masokwe: Hylobatidae (masokwe wadogo au giboni) na Hominidae (masokwe wakubwa wakiwemo binadamu).
Masokwe wadogo huishi daima mitini na huteremka kwa nadra. Wana mikono mirefu ili kining'inia kutoka tawi moja hadi jingine na kutoka mti mmoja hadi mwingine. Wanatokea misitu ya tropiki ya Asia.
Masokwe wakubwa hupitisha muda pengine mrefu ardhini, orangutanu muda kidogo tu na ngagi muda mrefu sana. Takriban spishi zote zinatokea Afrika lakini orangutanu wanatokea Asia ya Mashariki.
UainishoEdit
Familia ya juu Hominoidea (Masokwe)
- Familia Hylobatidae (Masokwe wadogo)
- Jenasi Hylobates (Hylobates)
- Jenasi Hoolock (Hoolock gibbon)
- Jenasi Nomascus (Nomascus)
- Jenasi Symphalangus (Siamang)
- Familia Hominidae (Masokwe wakubwa)
PichaEdit
Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.