Vivumishi vya pekee

Vivumishi vya pekee ni aina ya vivumishi ambavyo vimekuwa vikileta hali ya kutokuwa bayana kwa wanasarufi wengi.

Vitabu vingi vielezavyo dhana ya vivumishi hasa katika daraja la vivumishi vya pekee, waandishi wake yamkini hawajafanya uchunguzi wa kutosha.

Neno pekee katika aina hii ya vivumishi linatokana na aina ya nomino za pekee, hasa zile ambazo ni majina ya pekee ya mahali kama vile Afrika, Tanzania, Dar es Salaam, New York, London n.k. Kivumishi cha pekee kinachotokana na nomino ya pekee ya Afrika ni Muafrika kama tunazungumzia mtu au Kiafrika kama tunazungumzia kitu kisicho mtu. Tanzania inatupatia kivumishi cha pekee Mtanzania / Kitanzania. Uingereza inatupatia kivumishi cha pekee cha Mwingereza / Kiingereza n.k.

Hii ndiyo maana halisi ya aina ya vivumishi viitwavyo vya pekee.

Mifano katika sentensi: "Tafadhali nipimie mchele wa Kijapani kilo saba". "Utamaduni wa Kiafrika ni tofauti kabisa na utamaduni wa Kiulaya". "Nyimbo za Kinaijeria huimbwa katika lugha ya wazawa". Humo maneno: Kijapani (Japani), Kiafrika (Afrika) na Kiulaya (Ulaya) yametumika kama vivumishi vya pekee.

Ndiyo maana neno "pekee" katika "vivumishi vya pekee" limetumika kuonesha kuwa vivumishi hivi vimechimbuka kutoka "aina za nomino za pekee za mahali".

S. Mghulu [1] anakosa kutambua vivumishi vya pekee ingawa anataja kategoria nyingine za vivumishi kama vya idadi, sifa, viulizi, vionyeshi, vimilikishi na visisitizi.

Sababu ya kuitwa vivumishi "vya pekee" bado si bayana kwa mwandishi; hata hivyo, pengine jina hilo linatokana na lile la viwakilishi vya pekee [2], kwani vivumishi na viwakilishi vinakaribiana sana katika isimu (kwa sababu nomino ikiondolewa katika kishazi kilicho na kivumishi, kivumishi hubadilika na kuwa kiwakilishi).

Kwa mfano:

-Mama mwenye ameondoka (sentensi ina nomino na kwa hivyo "mwenye" ni kivumishi)

-Mwenye ameondoka (hapa neno "mwenye" ni kiwakilishi na si kivumishi tena)

Kwa hivo zifuatazo ni aina za vivumishi vya pekee:

-enye (Kiti chenye mbao kimetenyenezwa)

-ote (Mavazi yote ni yangu)

-o-ote (Nipe kamba lolote)

-enyewe (Mtu mwenyewe simjui)

-ingine (Siku nyingine utakuja)

Iwapo unatumia kivumishi cha pekee -enye, ni hatia kufuatwa na kitenzi. Kwa mfano: mtoto mwenye amekuja ataadhibiwa. Neno mtoto ni nomino ya kawaida - mwenye ni kivumishi cha pekee -enye - amekuja ni kitenzi. Njia sahihi ya kuandika sentensi hiyo ni: mtoto mwenye hatia ataadhibiwa. Yaani, -enye lazima ifuatwe na nomino.

Tanbihi hariri

  1. Mghulu, S. (1999), "Mtalaa wa Isimu", Longhorn Publishers: Nairobi, uk 156
  2. https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Viwakilishi_vya_pekee
  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vivumishi vya pekee kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.