Edmund Rich (Abingdon, Uingereza, 1174 hivi – Soisy-Bouy, Ufaransa, 16 Novemba 1240) alikuwa mwalimu maarufu wa hisabati, falsafa na teolojia katika vyuo vikuu vya Paris na Oxford, halafu mhubiri, na hatimaye askofu mkuu wa Canterbury.

Mt. Edmund katika mchoro mdogo.

Kwa juhudi zake alirekebisha umonaki, Kanisa la Uingereza na nchi kwa jumla[1].

Alitangazwa mtakatifu na Papa Inosenti IV tarehe 16 Desemba 1246.

Wakatoliki[2] na Waanglikana wanaadhimisha sikukuu yake tarehe ya kifo chake.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.