Irugwa ni kata ya Wilaya ya Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza, Tanzania.

Kata hiyo inaundwa na kisiwa cha Irugwa na visiwa vingine vidogo vya Kulazu, Buluza na Lyegoba.

Irugwa inavyo vijiji viwili Sambi (yalipo makao makuu ya kata) na Nabweko.

Kitongoji maarufu ni Buyanza (wenyewe wakijiita Washabunda) maana ndipo hasa zilipo huduma muhimu za jamii kama zahanati, ofisi ya kata, shule ya msingi na mitambo ya maji safi na maji taka bila kusahau mitambo ya kuzalisha umeme.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 13,314 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 11,873 waishio humo.[2] Msimbo wa posta ni 33624.

Kata ina shule za msingi tano ambazo ni Irugwa, Nabweko, Kulazu, Buluza na Lyegoba. Kuna shule ya sekondari moja iitwayo Irugwa.

Marejeo hariri

  Kata za Wilaya ya Ukerewe - Mkoa wa Mwanza - Tanzania  

BukandaBukikoBukindoBukongoBukunguBwiroBwisyaIgallaIlangalaIrugwaKageraKagunguliKakeregeKakukuruMukituntuMuritiMurutunguruNakatunguruNamagondoNamilembeNansioNdurumaNgomaNkilizyaNyamanga

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mwanza bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Irugwa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.