Lua error in package.lua at line 80: module 'Module:Navbar/configuration' not found. Konde ni jina la kihistoria kwa ajili ya Unyakyusa katika wilaya ya Rungwe nchini Tanzania na pia sehemu ya kaskazini ya Malawi kando la Ziwa Nyassa ambako umbo la jina ni "ngonde". Wenyeji wake waliitwa Wakonde tofauti na Makonde au Wamakonde wa Mkoa wa Mtwara.

Jina linaendelea kutumiwa hasa kwa ajili ya Dayosisi ya Konde ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania.

Kiasili maana ya kienyeji ya "Konde" ni tambarare na inamaanisha nchi tambarare kando ya Ziwa Nyassa upande wa kaskazini hadi milima ya Livingstone. Baadaye jina lilitumiwa pia kwa ajili ya maeneo yaliyokaliwa na Wakonde walioendelea kujenga vijiji kwenye mtelemko wa milima ya Rungwe na Uporoto inayopanda juu ya ncha ya kaskazini ya ziwa hilo.

Wakoloni Wajerumani waliitwa wakazi wote wa eneo hili "Konde" wakihesabu Wanyakyusa kama kundi kubwa kati yao.

Wakati wa utawala wa Waingereza jina la Unyakyusa lilianza kuwa kawaida kwa eneo lote upande wa Tanganyika.

Tazama pia

hariri

Marejeo

hariri
  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mbeya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Konde kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.