Leopoldo Bogdan Mandić, O.F.M.Cap. (Herceg Novi, Boka Kotorska, Montenegro, 12 Mei 1866 - Padova, Italia, 30 Julai 1942) alikuwa kwa asili mtu wa kabila la Wakorasya.[1]

Mt. Leopoldo Bogdan Mandić alivyoonekana kawaida, akiwa tayari kuungamisha waamini.

Ingawa mfupi sana (mita 1.35) na mlemavu, alistawi kiroho hasa baada ya kujiunga na utawa wa Ndugu Wadogo Wakapuchini na kufikia upadri (20 Septemba 1890).

Alitamani kwenda Ulaya Mashariki ili kurudisha umoja kati ya Wakatoliki na Waorthodoksi, lakini kwa utiifu aliishi karibu daima nchini Italia, na tangu mwaka 1906 hadi kifo chake alikuwa Padova akiungamisha mchana kutwa umati wa watu waliomuendea, wakivutiwa na wema wake[2].

Wakati wa Vita vikuu vya pili, mabomu yalibomoa konventi alimoishi na kanisa lake, lakini si chumba alimokuwa anaungamisha. Ndivyo alivyokuwa ametabiri, "Hapa Mungu ametumia sana huruma yake kwa watu wengi, lazima pabaki kama ukumbusho wa wema wake".

Papa Paulo VI alimtangaza mwenyeheri tarehe 2 Mei 1976, halafu Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu tarehe 16 Oktoba 1983.

Sikukuu yake huadhimishwa kila tarehe 30 Julai[3] au 12 Mei.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Veliki svetac i rodoljub, Bogdan Leopold Mandić (Croatian). hkv.hr (23 August 2010). Iliwekwa mnamo 11 May 2013. “Tijekom Drugog svjetskog rata proveo je godinu dana u talijanskom zatvoru ne želeći poreći svoju hrvatsku nacionalnost.”
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/52950
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.