Historia ya Kamerun

Historia ya Kamerun inahusu eneo la Afrika ya Kati ambalo wakazi wake leo wanaunda Jamhuri ya Kamerun.

Historia ya awali hariri

Katika karne za BK Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi walianza uenezi wao kutoka huko kwenda kutawala maeneo mengi ya Afrika ya Kati, Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki.

Wakati wa ukoloni hariri

Kamerun ilikuwa koloni la Ujerumani hadi Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baada ya Ujerumani kushindwa vita, nchi ikagawiwa kati ya Uingereza na Ufaransa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa kama eneo la kukabidhiwa.

Tangu uhuru hadi leo hariri

Mwaka wa 1960, Wafaransa waliacha Kamerun ikawa nchi huru. Wananchi wa Kamerun ya Kiingereza walipiga kura kuamua kama walitaka kuwa sehemu ya Nigeria au ya Kamerun. Kaskazini wengi walipendelea kukaa Nigeria, hivyo maeneo hayo sasa ni sehemu ya Nigeria. Wananchi wengi wa kusini waliamua wajiunge na Kamerun[1]. Kwa kusudi la kuheshimu tofauti za kiutamaduni kulikuwa na katiba mpya kwenye mwaka 1961 Shirikisho la Jamhuri ya Kamerun.

Tangu 1972 muundo wa nchi ulibadilishwa kuacha mfumo wa shirikisho na kuwa jamhuri ya muungano inayokazia zaidi matumizi ya lugha ya Kifaransa ingawa Kiingereza bado ni moja ya lugha rasmi. Jina la nchi pia likabadilishwa kuwa Jamhuri ya Muungano ya Kamerun mwaka wa 1972. Hapo sehemu ya Wakamerun wanaotumia lugha ya Kiingereza walijisikia kuwa wananyimwa haki zao.[2] Baadaye, mwaka wa 1984 jina likabadilishwa tena kuwa Jamhuri ya Kamerun (kwa Kifaransa République du Cameroun).

Tangu mwaka 2016 upinzani wa watu wa magharibi ulijibiwa kwa ukali zaidi na hii imeleta upinzani wa wanamgambo wenye silaha wanaoshambulia polisi na jeshi la serikali kuu. Tangu mwaka 2017 wapinzani wamedai uhuru wa sehemu yenye lugha ya Kiingereza wakidai kuundwa kwa nchi ya Ambazonia.

Tarehe 5 Januari 2018, washiriki wa serikali ya mpito ya Ambazonia, pamoja na Rais Sisiku Julius Ayuk Tabe, walikamatwa nchini Nigeria na kupelekwa nchini Kamerun. Walikamatwa baadaye na kuishiwa miezi 10 katika makao makuu ya gendarmerie kabla ya kuhamishiwa gereza la usalama la juu huko Yaoundé. Kesi ilianza Desemba 2018.

Tarehe 4 Februari 2018, ilitangazwa kuwa Bwana Samuel Ikome Sako atakuwa Rais Kaimu wa Shirikisho la Ambazonia, kufanikiwa kwa muda kwa Tabé. Urais wake uliona kuongezeka kwa vita na kuenea kwake kwa kusini mwa Kamerun. Tarehe 31 Desemba 2018, Ikome Sako alitangaza kuwa mwaka 2019 utaona mabadiliko kutoka kwa vita ya kujihami kwenda vita ya kukera na kwamba watengwa watajitahidi kupata uhuru katika ardhi.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. 1961 British Cameroons Plebiscite, kwenye tovuti ya africanelections.tripod.com/referenda, iliangaliwa Januari 2019
  2. Anglophone crisis: Cameroon must return to federal system abolished under Ahidjo, Abdur Rahman Alfa Shaban kwenye tovuti ya africanews.com tar. 11/03/2018
  Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Kamerun kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.