Nona wa Nazianzo (305 hivi - 374 hivi) alikuwa mke wa Gregori Mzee na mama wa Gregori wa Nazianzo, Sesari wa Nazianzo na Gorgonia wa Nazienzi. Aliishi huko Kapadokia, mkoa wa Dola la Roma katikati ya Uturuki wa leo.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu pamoja na familia yake yote.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 5 Agosti[1].

Maisha hariri

Baada ya kuolewa , Nona alimsaidia Gregori mumewe kuongokea Ukristo kutoka madhehebu yenye mchanganyiko wa Uyahudi na Upagani yaliyomuabudu Hypsistos, Mungu "Aliye Juu".

Aliishi mpaka baada ya kifo cha mumewe, aliyefikia uaskofu, na ya wanae wawili.[2]

Mwanae maarufu zaidi, Gregori, ambaye pia alifikia uaskofu na anaheshimiwa kama mwalimu wa Kanisa, alitangaza sifa za mamaye[3]

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Martyrologium Romanum
  2. Jones, Terry. "Nonna". Patron Saints Index. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2007-03-22. Iliwekwa mnamo 2007-05-06. 
  3. My mother was a worthy companion for such a man [as my father] and her qualities were as great as his. She came from a pious family, but was even more pious than they. Though in her body she was but a woman, in her spirit she was above all men... Her mouth knew nothing but the truth, but in her modesty she was silent about those deeds which brought her glory. She was guided by the fear of God...Rabenstein, Katherine (August 1998). "Nonna of Nazianzen, Matron". Saints O' the Day for August 5. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo February 6, 2007. Iliwekwa mnamo 2012-02-23.  Check date values in: |date=, |archivedate= (help)

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.