"Regina caeli" (tamka: reˈdʒina ˈtʃeli; maana yake Malkia wa Mbingu)ni antifona inayotumika kumuelekea Bikira Maria katika Kanisa la Kilatini wakati wa Pasaka, kuanzia Dominika ya Ufufuko wa Yesu hadi Pentekoste.

Antifona ikiimbwa.
Nota za Regina caeli[1]

Katika siku hizo hamsini ndiyo antifona pekee inayotumika kumalizia Sala ya mwisho ya Liturujia ya Vipindi [2] lakini pia inashika nafasi ya sala ya Angelus (inayofanyika mara tatu kwa siku: asubuhi, adhuhuri na jioni).

Maneno asili kwa Kilatini hariri

  • Regina caeli, laetare, alleluia;
  • Quia quem meruisti portare, alleluia,
  • Resurrexit, sicut dixit, alleluia:
  • Ora pro nobis Deum, alleluia.[3]

Tafsiri ya Kiswahili hariri

  • Malkia wa mbingu, furahi, aleluya;
  • Kwani uliyestahili kumchukua, aleluya,
  • Amefufuka, alivyosema, aleluya:
  • Utuombee kwa Mungu, aleluya.[4]

Historia hariri

Mtunzi wa Regina caeli hajulikani. Kimaandishi inapatikana katika kitabu cha antifona cha mwaka 1200 hivi kinachotunzwa katika Basilika la Mt. Petro, huko Vatikani, jijini Roma.[5]

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. The Regina caeli sung. Youtube. Re-accessed Oct 2021.
  2. "Finally one of the antiphons of the Blessed Virgin Mary is said. In Eastertide this is always the Regina caeli" (General Instruction of the Liturgy of the Hours, p. 18, paragraph 92).
  3. Loyola Press: Regina Caeli. Re-accessed Oct 2021.
  4. Misale ya waamini, toleo la mwaka 2021.
  5. Heinz, Andreas (1997). Walter Kasper, mhariri. Marianische Antiphonen. Lexikon für Theologie und Kirche 6 (toleo la 3) (Freiburg im Breisgau: Verlag Herder). uk. 1358. ISBN 9783451220012. Iliwekwa mnamo 15 October 2021.  Unknown parameter |lang= ignored (|language= suggested) (help); Check date values in: |accessdate= (help)

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: