Vyakula vibadilishaji

vyakula vinavyozalishwa kutoka kwa viumbe ambavyo vimeleta mabadiliko katika DNA zao

Vyakula vibadilishaji (pia kujulikana kama vyakula vilivyoboreshwa) ni vyakula ambavyo vilitengenezwa kutokana na viumbehai ambao wamebadilishwa katika DNA kwa kutumia uhandisi wa maumbile.

Mahindi.
Kahawa.
DNA UV mutation ta.

Mbinu za uhandisi huo zinahurusu kudhibiti sifa za maumbile ya hivyo vyakula viliyoboreshwa. Hii ni aina mojawapo ya kubadilisha maumbile, badala ya kuchagua uzalishaji au kuzaliwa kwa mabadiliko.

Duniani, kuna makubaliano ya kisayansi kwamba vyakula viliyoboreshwa visiwe na hatari kubwa zaidi kwa afya ya binadamu vikilinganishwa na vyakula vya asili, lakini, badala ya kuwasilisha vyakula viliyoboreshwa katika masoko, vinafaa kupimwa na vyakula vya asili na kushughulikia tofauti katika vyakula hivyo.

Historia hariri

Vyakula vilivyoboreshwa vilianza na kuchagua mbegu au wanyama kuzaliana kwa sababu ya kupenda tabia za wanyama au vyakula hivyo, na wafugaji walitaka kuendeleza urithi za hizo tabia. Kuchagua uzalishaji kulianza vyakula vilivyoboreshwa, halafu katika miaka ya 1900, wanasayansi waligundua DNA na namna ya kubadilisha sehemu zake, hivyo walianza kutumia uhandisi wa maumbile badala ya kutumia uzazi wa kuchagua. Kutumia uhandisi wa maumbile ni bora kuliko uzazi wa kuchagua kwa sababu uzazi wa kuchagua hukua na tabia nyingine pamoja na tabia ambayo wafugaji walipenda. Lakini kwa sababu walifaa kuzalishwa na tabia zote, ilikuwa vigumu kutoa tabia ambazo hawakupenda. Lakini uhandisi wa maumbile huweza kutoa na kuongeza tabia zote ambazo wafugaji hupenda au hawapendi, bila kuzalishwa mara kwa mara hadi kupata viumbe kamili.

Mimea iliyoboreshwa katika nchi za Afrika Mashariki hariri

Katika nchi za Afrika Mashariki, uhalali na udhibiti wa hali ya vyakula vilivyoboreshwa una tofauti kati ya nchi, kwa sababu nyingine hazitaki vyakula vibadilishaji, wakati nchi nyingine zinavikubali sana.

Katika idara ya kilimo katika nchi ya Kenya, watu wanapenda vyakula viliyoboreshwa kwa sababu nchi ya Kenya huleta uchumi wa kilimo kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki, pia huweza kulima vyakula vingi kutokana na uhandisi wa maumbile. Wanaweza kufanya hivyo kwa kubadili sehemu za DNA na hivyo wanaweza kutengeneza vyakula vinavyoweza kufanya vitu vingi. Kwa mfano, nafaka zinazohitaji maji saa zote, kwa msaada wa uhandisi wa maumbile, hazihitaji maji saa zote na wanaweza kukuza vyakula vizuri pia.

Mmea moja ambao ulibadilishwa ni pamba. Pamba katika nchi ya Kenya ni mmea mkuu kwa sababu watu wanapenda kutumia pamba kutengeneza nguo. Sasa hivi, kwa kubadilisha DNA katika pamba, pamba huweza kupinga magonjwa na wadudu wenye kuharibu mimea ya pamba.

Mimea mingine ambayo ilibadilishwa ni kahawa, mahindi, muwa, na chai. Hubadilishwa DNA za mimea kwa sababu wafugaji hawapendi kutumia dawa kuzuia wala mimea. Sasa hivi, badala ya kutumia dawa, wafugaji hutumia uhandisi wa maumbile kuwazuia na mimea haiharibu mazingira karibu nayo, lakini wadudu hawali mimea pia.

  Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vyakula vibadilishaji kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.