Waraka wa pili kwa Timotheo

Agano Jipya

Barua ya pili kwa Timotheo ni kimojawapo kati ya vitabu 27 vya Agano Jipya katika Biblia ya Kikristo. Ni moja ya kundi la Nyaraka za Kichungaji.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Mwandishi ni Mtume Paulo akiwa kifungoni Roma kwa mara ya mwisho, muda mfupi kabla ya kukatwa kichwa wakati wa dhuluma (64-67 B.K.) ya Kaisari Nero dhidi ya Wakristo.

Maneno yake ya buriani yanaonyesha tumaini lake ambalo alikabili hicho kifodini.

Viungo vya nje hariri

Tafsiri ya Kiswahili hariri

Vingine hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya Agano Jipya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Waraka wa pili kwa Timotheo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.