Waraka wa pili kwa Wathesaloniki

Waraka wa pili kwa Wathesalonike ni kati ya vitabu 27 vya Agano Jipya katika Biblia ya Kikristo.

Wongofu wa Mtume Paulo akielekea Damasko (mchoro ≥wa Caravaggio).
Agano Jipya

Ni barua ya Paulo wa Tarso kwa ushirika wa Wakristo katika mji wa Thesalonike (Ugiriki wa Kale).

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Mazingira hariri

Miezi michache baada ya Mtume Paulo kuwaandikia Wakristo wachanga wa Thesalonike barua tulivu, akarudia kuwaandikia kutokana na taarifa nyingine zilizomtia tena wasiwasi.

Akawafafanulia zaidi Ujio wa pili wa Bwana na dalili zake, akiwahimiza hasa kufanya kazi kwa bidii na kuwajibika wakati wa kungojea ujio huo wa Yesu badala ya kuiacha kwa kisingizio cha kwamba, eti Kristo amesharudi (2Thes 2:1-15; 3:6-15).

Mpangilio hariri

Mpangilio wa barua hizo ni uleule wa barua zitakazofuata: baada ya salamu na shukrani kwa Mungu, yanafuata mafundisho ya imani, halafu maadili, na hatimaye salamu nyingine.

Marejeo hariri

  • Buttrick, George Arthur; Bowie, Walter Russell; Scherer, Paul; Knox, John; Bailey Harmon, Nolan; Terrien, Samuel, eds. (1955), The Interpreter’s Bible 11th, Nashville: Parthenon Press 
  • Brown, Raymond; Collins, Raymond; Murphy, Roland, eds. (1990), The New Jerome Biblical Commentary, Englewood Cliffs, NJ: Prentice Hall 
  • Clarke, Adam (1831), The New Testament of our Lord and Saviour Jesus Christ 2nd, New York: Methodist Episcopal Church 

Viungo vya nje hariri

 
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:

Tafsiri ya Kiswahili hariri

  • [1] Agano Jipya kwa lugha ya Kiswahili

Vingine hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya Agano Jipya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Waraka wa pili kwa Wathesaloniki kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.