Yohane Southworth (Lancashire, Uingereza, 1592 hivi – Tyburn, London, 28 Juni 1654) alikuwa Mkristo wa Kanisa Katoliki pamoja na familia yake wakati wa dhuluma ya nchi hiyo iliyotaka wote wawe Waanglikana[1].

Mt. Yohane Southworth katika mavazi ya ibada.

Baada ya kuhamia Ufaransa, aliingia seminari kwa kengo la kurudi kwao kufanya uchungaji usioruhusiwa na serikali. Kisha kupewa daraja ya upadri alifaulu kufanya utume Uingereza miaka 1619-1624[2] na 1626-1627[3].

Ndipo alipokamatwa na kukaa gerezani hadi mwaka 1630 alipofukuzwa nchini badala ya kuuawa kama alivyohukumiwa.

Mwaka 1636 alikuwa amerudi London akawa anahudumia wagonjwa wa tauni[4]. Kati ya miaka 1637 na 1640 mara nne alikamatwa na kuachwa au kutoroka akiendelea na utume kwa siri hadi mwaka 1654 aliponyongwa na kukatwakatwa chini ya sheria ya serikali ya Oliver Cromwell. Akitazama kamba aliyoandaliwa alisema ilikuwa kwake kama msalaba wa Yesu[5].

Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri mwaka 1929. Halafu Papa Paulo VI tarehe 25 Oktoba 1970 akamtangaza kuwa mtakatifu mfiadini pamoja na wenzake 39.

Sikukuu yake ni tarehe 28 Juni[6].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.